Jul 22, 2016

Wanafunzi wakosa masomo kwa ukosefu wa vyoo


Wanafunzi wakiangalia vyoo wanavyovitumia

Wanafunzi wa Shule ya msingi Maendeleo Manispaa ya Mtwara Mikindani wanalazimika kukosa sehemu ya vipindi vya masomo darasanai kutokana na kupanga foleni kusubiri zamu ya kwenda kujisaidia chooni.
Wakizungumza shuleni hapo, wamesema kuwa hali hiyo inatokana na shule yao kutokuwa na vyoo, hivyo wanalazimika kwenda kutumia vyoo vya shule jirani ya Rahaleo ambayo pia inakabiliwa na upungufu wa matundu ya vyoo.
Kwa upande wa walimu wa shule zote mbili, wamesema changamoto ya miundombinu ni kubwa katika shule hizo huku na wao ambao idadi yao jumla ni Zaidi ya 40 wakitumia matundu mawili ya choo cha shule moja, na kuiomba serikali na wadau wengine kuona umuhimu wa kutatua changamoto hizo.
Naibu Meya wa manispaa hiyo, Erick Mkapa ambaye ni diwani wa kata ya Rahaleo, amekiri kuwapo kwa changamoto hiyo na kueleza kuwa anafanya juhudi za kuwashirikisha wadau mbalimbali kwa ajili ya kuhakikisha wanatatua tatizo hilo.