Wanariadha
wanne watakao iwakilisha Tanzania katika Michuano ya Olyimpiki nchini
Brazil wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la
Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi pamoja na Rais wa Shirikisho la
Riadha Tanzania (RT) Antony Mtaka ,wengine kutoka kulia ni Mkufunzi wa
wanariadha hao,Francis John na anyefuatia ni Mkurugenzi wa Utalii na
Masokowa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa.
Meneja
Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete
akitoa neno la ukaribisho kwa wanahabari na wageni wengine katika hafla
fupi ya kukabidhi hundi kwa wanariadha wanaounda timu ya taifa,
inayojiandaa na mashindano ya Olimpiki yatakayoafanyika mwezi Agosti
nchini Brazil.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi,akizungumza
wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi ya Shilingi Milioni tano kwa
wanariadha wanaounda timu ya taifa inayojiandaa na mashindano ya
Olimpiki.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akikabidhi
mfano wa hundi ya Shilingi Milioni tano kwa Rais wa Shirikisho la Riadha
Tanzania (RT) Anthony Mtaka kwa ajili ya kusaidia wanariadha wanaounda
timu ya taifa wakijiandaa na mashindano ya Olimpiki. 
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akikabidhi
"Track Suit "maalumu zenye maandishi na nembo yanayotangaza vivutio vya
utalii vilivyopo nchini kwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT)
Anthony Mtaka kwa ajili ya kusaidia wanariadha wanaounda timu ya taifa
wanaojiandaa na mashindano ya Olimpiki.