Jul 15, 2016

JAJI MKUU WA TANZANIA, ZIARANI MAHAKAMA KANDA YA MOSHI, AZINDUA RASMI MAHAKAMA ZA MWANZO BOMANG’OMBE NA SIHA.

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa Mahakama Kanda ya Moshi mara baada ya uzinduzi rasmi ya Mahakama ya Mwanzo Boang’ombe wilayani 
 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman, akilakiwa na Mhe. Aishieli Sumari, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Moshi alipowasili Mahakamani hapo kwa ziara ya kikazi ya kujionea hali ya utendaji kazi katika Kanda hiyo.
 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Moshi.
 Mhe. Jaji Mkuu akisalimiana na baadhi ya Watumishi wa Mahakama, Kanda alipowasili mapema Julai 14, 2016 kwa ziara ya kikazi.
 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Mahakama ya Mwanzo Bomang’ombe iliyopo Wilayani Siha Manispaa ya Moshi.