Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akimsikiliza Kelvin Agustino mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya Msingi ya Mchepuo wa Kiingereza ya Katavi iliyopo Mikwambe, Kigamboni Wilayani Temeke alipokuwa akisoma kitabu cha Kiingereza wakati alipoitembelea shule hiyo hivi karibuni ili kuwasalimia wanafunzi na kujionea maendeleo ya shule hiyo.
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akiwauliza maswali wanafunzi wa shule ya awali wa shule ya Msingi ya Mchepuo wa Kiingereza ya Katavi iliyopo Mikwambe, Kigamboni Wilayani Temeke wakati alipotembelea shule hiyo hivi karibuni ili kuwasalimia wanafunzi na kujionea maendeleo ya shule hiyo.