Rais
wa kikundi cha Upendo Women's Group ambaye pia ndiye mwenyekiti cha
kikundi hicho Mh:Theresia Greca,ametoa shukrani za dhati kabisa kwa Rais
mstaafu wa Tanzania Mh: Benjamin William Mkapa kwa kuwachangia kikundi
chao,Shukrani za pekee kwa Kaimu Balozi wa Tanzania Mrs Agnes Kayola na
Ubalozi mzima kwa mchango wao mkubwa wa kufanikisha zoezi zima la
ufanikishaji wa fedha za kuisaidia hospital ya Mwananyamala nchini
Tanzania.{picha na maelezo toka Maganga One Blog}
Pichani
wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali waliohudhuria sherehe za
uchangishaji wa fedha kwa ajili ya hospitali ya Mwananyamala ya jijini
Dar es Salaam.Shukrani zinatolewa na wana Upendo Women's Group kwa
ufanikishaji wa zoezi zima
Baadhi
ya Viongozi na wanachama wa Upendo Women's Group,kina mama wenye makazi
yao nchini Ubegiji wametoa shukrani zao za dhati kabisaa kwa kila mmoja
alishiriki vyema katika kufanikisha shughuli yao ya uchangishaji wa
fedha kwa ajili ya kuisadia hospitali ya Mwananyamala ya jijini Dar es
Salaam nchini Tanzania.Wana Upendo wanapeleka shukrani zao kwa Rais
Mstaafu Mh:Benjamin William Mkapa kwa kujitolea mchango wake,Bila
kusahau shukrani zao kwa Kaimu Balozi wa Tanzania Mrs Agnes Kayola na
Ubalozi mzima wa Tanzania nchini Ubelgiji.Wanatoa shukrani kwa vikundi
mbalimbali vya maonyesho na kila mmoja aliyefanikisha zoezi zima.
Katika
kuchangisha fedha ili kusaidia hospitali ya Mwananyamala nchini
Tanzania, Upendo Women's Group waliaanda maonyesho mbalimbali ikiwemo na
maonyesho ya mavazi.
Afisa
Ubalozi Mr.Shayo {kushoto} pia nae alishiriki katika sherehe hizi fupi
za uchangishaji wa pesa wa kuisaidia hospital ya Mwananyamala ya jijini
Dar es Salaam.Wana Upendo Group wanatoa shukrani zao za dhati kwa
ushiriki na mchango wao mkubwa waliojitolea wa maafisa ubalozi wa
Tanzania katika kufanikisha zoezi zima.