Mkuu
wa Wilaya ya Ilala Mh. Raymond Mushi, akisaidiana na Mwenyekiti wa
Banki ya Diamond Trust (DTB), Bw. Abdul Samji, kukata utepe katika
uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo la CBD. Kushoto ni Bi. Nasim Devji
Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo nchini, kulia ni Mwakilishi wa Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam, Hezron Gyimri. Tawi la CBD linakuwa ni tawi la
25 la benki hiyo nchini Tanzania na la 11 jijini Dar es Salaam.
Benki
ya Diamond Trust Tanzania, (DTB Tanzania),leo imezindua rasmi tawi la
CBD lilipolo katikati ya jiji la Dar es Salaam kwenye jengo la Diamond
Plaza, makutano ya barabara ya Samora na mtaa wa Mirambo. Tawi la CBD ni
la ishirini na tano nchini na la kumi na moja katika jiji la Dar es
Salaam.
Tawi
la CBD litafunguliwa jumatatu hadi ijumaa, saa 2:30 asubuhi hadi saa
10:30 jioni na Jumamosi saa 3:30 asubuhi hadi sa 7:00 mchana.
Akihutubia
katika hafla fupi iliyofanyika ndani ya benki, Mgeni rasmi ambaye ni
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Raymond Mushi, alitoa pongezi kwa
uongozi wa benki ya DTB Tanzania kwa ufunguzi wa takriban matawi mawili
kila mwaka licha ya changamoto zinazokabili sekta ya fedha nchini na
duniani kwa ujumla. Benki ya DTB imefanikiwa kufungua matawi ishirini na
moja katika miji kumi na tatu ndani ya mika minane (2007 – 2016).
