Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong un
RAPA maarufu wa Marekani Nicki Minaj,
rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong un, msaka tiketi ya kuwania urais
Marekani kwa tiketi ya Republican Donald Trump na Lewis Hamilton wana
kitu kimoja kinachowaunganisha. Huwezi kufikiria kwamba wanaweza kuketi
katika meza moja, lakini wametajwa miongoni mwa watu 100 wenye ushawishi
mkubwa duniani.
Donald Trump
Orodha hiyo ya mwaka 2016 pia
inamshirikisha Hillary Clinton, Kendrick Lamar, PewDiePie, Adele,
Caitlyn Jenner na Leonardo DiCaprio.
Katika tamasha la siku ya Jumanne la New
York baadhi ya nyota hao walihudhuria. Nicki alisema kuwa hiyo
inatokana na yeye kuwa mwanamke huru huku akiwaambia wanaume waliojaa
katika ukumbi wa tamasha hiyo kwamba: iwapo hamjui kuwashughulikia
wanawake wenu kuna watu 100 ambao wana uwezo wa kuchukua fursa hiyo.
Nicki Minaj
Lewis Hamilton alisema kuwa ni heshima
kubwa kwake kuorodheshwa katika tamasha hiyo ya watu 100 mbali na
kuorodheshwa miongoni mwa watu 100 duniani walio na ushawishi mkubwa.
Wakati huohuo alimuomboleza marehemu Prince akisema kuwa alikuwa mwanamuziki bora wa kizazi chote