Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga akitoa pole kwa niaba ya Wizara kwa familia ya aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Marehemu Balozi Joseph Rwegasira wakati wa ibada ya mazishi iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Jijini Dar es Salaam.Balozi Mahiga alimwelezea Marehemu Balozi Rwegasira kuwa alikuwa kiongozi hodari wa kupigiwa mfano kutokana na moyo wake wa kufanya kazi kwa bidii na kujituma.
Ndugu na jamaa waliohudhuria ibada hiyo wakimsikiliza kwa makini Waziri Mahiga (hayupo pichani).
Sehemu nyingine ya watu waliohudhuria ibada hiyo .
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Jaji Joseph Sinde Warioba naye alipata fursa ya kutoa neno la pole kwa familia ya Marehemu Balozi Rwegasira.
Mmoja wa wanafamilia ya Balozi Rwegasira akisoma utaratibu wa kutoa heshima za mwisho za kuuaga mwili wa Balozi Rwegasira .
Sehemu ya Viongozi wa Serikali na Vyama vya Kisiasa wakisikiliza utaratibu wa kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Balozi Rwegasira.