
Ndege
ya uzinduzi ya Shirika la Ndege la Etihad ikipokelewa na magari ya
zimamoto ambayo yalimwaga maji kuashiria uzinduzi rasmi wa Safari za
ndege kati ya Rabat na Abudhabi.
Safari kati ya Abu Dhabi na Morocco kufikia tisa kwa wiki
Shirika
la ndege la Etihad lazindua rasmi huduma zake za ndege baina ya Abu
Dhabi na Rabat, Morocco, ikiwa ni kituo chao cha pili nchini humo.
Ndege
ya uzinduzi iliwasili mchana wa leo uwanja wa ndege Sale-Rabat na
kupokelewa na mzinga wa maji kama ilivyo desturi ikifuatiwa na wageni
rasmi kuwasili, wakiwemo; Lahcen Haddad (Waziri wa Utalii Morocco), na
Balozi wa UAE kwa Morocco, Mh. Al Asri Saeed Al Dhaeri.
Huduma
hii itakayopatikana mara mbili kwa wiki kupitia ndege aina ya Airbus
A340-500 itakuwa yakipekee baina ya Rabat na Abu Dhabi. Tayari kukiwa na
safari baina ya Abu Dhabi na Casablanca, shirika litafikisha jumla ya
safari tisa kwa wiki kwenda nchini Morocco
Ndege
ya uzinduzi (EY615) kwenda Rabat ilibeba msafara ulioongozwa na Khaled
Al Mehairbi, Makamu Rais Mambo ya Serikali na Siasa za Anga. Uwakilishi
huu ulijumuisha Kapteni Salah Awadh Alfarajalla, Makamu Rais Usalama na
Maaendeleo ya Waendesha Ndege Kitaifa; Hareb Mubarak Al Muhairy, Makamu
Rais Mambo ya Mashirika na Kimataifa; Ali Al Shamsi, Makamu Rias
Operesheni za Kitovu cha Abu Dhabi; Joost Den Hartog, Kaimu Makamu Rais
wa Mauzo Duniani; na Amer Khan, Makamu Rais Mashariki ya Kati na Africa
Kaskazini.
James
Hogan, Rais na Mkurugenzi Mkuu wa Etihad, alisema shirika limefurahishwa
na uzinduzi wa huduma ya Rabat kama kituo cha pili katika safari za
Morocco.
“Safari
hizi mpya zitakazounganisha miji hii zinadhihirisha dhamira ya Etihad
kuendelea kujenga mahusiano endelevu na kanda ya ksakazini mwa Afrika na
kuimarisha uhusiano kati ya Morocco na Umoja wa Falme za Kiarabu,”
alisema.
“Rabat
ni mji wa kihistoria unaovutia wanaosafiri kwa ajili ya burudani na
biashara. Kwa kupitia huduma yetu mpya, tunalenga kutumia mtandao wetu
uliopo duniani kote kukuza wingi wa wasafiri wataotumia njia hii kuingia
Morocco. Vivyo hivyo tunarahisisha safari katika Rabat hadi Abu Dhabi
pamoja na miji mingine tunayofika, huku tukiwapa wageni wetu fursa ya
kufurahia huduma zetu za viwango vya juu zinazotambulika dunia nzima.”
Pamoja na Casablanca, huduma hii ya Rabat itafikisha jumla wasafiri 4,200 kila wiki kwenda Morocco.
Kama
UAE, serikali ya Morocco imewekeza sana katika kuiendeleza sekta ya
utalii. Mwaka 2010, serikali ilizindua Vision 2020 ikiwa na mpango wa
kuifanya Morocco kuwa kati ya sehemu kuu 20 za utalii duniani na hii
itachangia kuongeza idadi ya watalii hadi mara mbili ya idadi ya awali
hadi kufikia takribani milioni 20 mpaka kufika mwaka 2020.