Oct 18, 2015

WATUMISHI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE WAMUAGA RAIS KIKWETE


Picha zote za juu zikimuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Viongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje wakati alipowasili kwenye Kituo cha Kimataifa cha cha Mikutano cha Julius Nyerere ambapo Wizara ya Mambo ya Nje ilifanya hafla ya kumuaga Mhe. Rais.
Rais Kikwete akifunua kitambaa ambapo nyuma yake kuna picha ya Jengo la Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje linalokusudiwa kuanza kujengwa hivi karibuni. Rais Kikwete alifunua kitambaa hicho kuashiria kuanza ujenzi wa jengo hilo.
Rais Kikwete akipiga makofi kuonesha furaha yake kuwa Wizara ya Mambo ya Nje itapata ofisi za kisasa hivi karibuni
Rais Kikwete akiongozwa kuelekea ukumbi ulioandaliwa kwa ajili ya kufanya hafla ya kumuaga. Wanaomuongoza ni Waziri wa Mambo ya Nje na Uhirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe wa kulia kwa Rais Kikwete na Katibu Mkuu, Balozi Liberata Mulamula.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga akitoa neno la kuwakaribisha wageni waalikwa akiwemo Rais Kikwete katika hafla ya kumuaga.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Liberata Mulamula akitoa utambulisho wa wageni waalikwa wakiwemoWaheshimiwa Mabalozi waliostaafu.
Balozi Mstaafu akisalimia wajumbe baada ya kutambulishwa
Watumishi wa Wizara wakiwemo Wakuu wa Idara/Vitengo, Waheshimiwa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi wakiwa wameketi kwa ajili ya kushuhudia matukio ya hafla ya kumuaga Rais Kikwete.