Baadhi ya wanaCCM na wananchi
waliojitokeza kumsikiliza Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) katika mkutano
wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika Jimbo la Mwibara, Wilaya ya
Bunda, jana.
Sehemu ya wananchi wakiwa katika mkutano wa mgombea mwenza wa CCM, Jimbo la Mwibara.
Mgombea ubunge wa Jimbo la
Mwibara, Alphaxard Kangi Lugola akiwahutubia wanaCCM na wananchi wapenzi
wa chama hicho waliokuwa katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa
CCM, Bi. Suluhu jana Jimbo la Mwibara.
Mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia
Suluhu Hassan akizungumza na wananchi na wanaCCM Mji wa Mugumu, Wilaya
ya Serengeti jana. Ambapo katika hotuba yake amewahakikishia wananchi wa
eneo hilo kuwa muda mfupi baada ya kuingia madarakani atatoa maelekezo
kwa waziri wa kazi kuhakikisha makampuni yaliyowekeza Serengeti yanatoa
ajira bila upendeleo huku wakizingatia kutoa kipaumbele kwa
wanaSerengeti.

Wananchi na wanaCCM Mji wa Mugumu, Wilaya ya Serengeti wakiwa kwenye mkutano wa kampeni.
Mmoja wa mwangalizi maalumu wa
masuala ya Uchaguzi Mkuu akiendelea na kazi katika mkutano wa kampeni wa
CCM uliofanyika Mugumu jana.
Baadhi ya wananchi wa Jimbo la
Mwibara wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, kusikiliza
kilio chao njiani alipokuwa akielekea katika mkutano wa kampeni.
Wananchi hao kilio chao ilikuwa ni kuiomba Serikali iharakishe mchakato
wa kuipa hadhi ya wilaya Jimbo la Mwibara ili kusogezewa huduma anuai.
Mgombea
mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu
Hassan (hayupo pichani) akiwahutubia baadhi ya wanaCCM na wananchi
waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika
Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda.
Sehemu
ya umati katika mkutano wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) akiwahutubia
baadhi ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara
Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda.
Sehemu
ya umati katika mkutano wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) akiwahutubia
baadhi ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara
Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda.
Sehemu ya msafara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu pamoja na viongozi, wa CCM wakiwa meza kuu.
Imeandaliwa na mtandao wa thehabari