Mgombea
mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu Hassan
akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa
Mwasenge, Jimbo la Musoma Mjini. Katika hotuba yake aliwaomba wanaMusoma
kuichagua CCM ili iweze kuunda Serikali kwani imepanga kuboresha huduma
mbalimbali za kijamii pamoja na ujenzi wa miundombinu eneo hilo
itakayochangia kukua kwa biashara anuai. Alisema Serikali
itakayoundwa na CCM imepanga kujenga maeneo ya kisasa ya maegesho ya
meli (magati) Musoma na ndani ya miezi mitatu huduma ya maji maeneo
mbalimbali itapatikana kwa uhakika kutokana na kukamilika kwa mradi wa
maji eneo hilo. Aliongeza pia ili kuboresha huduma za Mwisenge zahanati
ya eneo hilo itabadilishwa mara moja na kuwa kituo cha afya. |