Madam Rita amedai kuwa pamoja na Runtown anayetamba kwa sasa na wimbo wake ‘Banger’ alioshirikiana na Uhuru, wasanii wengine watakaopanda jukwaani kutumbuiza ni Christian Bella, Yamoto Band, Navy Kenzo, Peter Msechu na Kala Jeremiah.
Runtown amewahi kuonesha nia ya kuurudia wimbo ‘Wanjera’ wa Ommy Dimpoz.
Fainali za shindano hilo zitafanyika Ijumaa ya October 9 kwenye ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga jijini Dar es Salaam.