Sep 4, 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. AFUNGUA KONGAMANO LA AFRIKA KUHUSU MAKUBALIANO YA RASIMU MPYA YA DUNIA, JIJINI DAR.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Kongamano la Afrika kuhusu Makubaliano ya Rasimu mpya ya Dunia inayohusu Usimamizi wa Masuala ya Tabianchi. Kongamano hilo lilianza jana Sept 3, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar esSalaam. 
 Baadhi ya Washiriki wa Kongamano hilo wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati akihutubia.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mh.  Dianna Melrose, wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Afrika kuhusu Makubaliano ya Rasimu mpya ya Dunia inayohusu Usimamizi wa Masuala ya Tabianchi. Kongamano hilo lilianza jana Sept 3, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar esSalaam.