Pichani
ni muonekano wa Banda la Shirika la Umoja wa Mataifa Tanzania ndani ya
Karume Hall katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara ‘Sabasaba’,
ndani ya viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
Pichani ni wananchi wakitembelea banda hilo na kupata taarifa
mbalimbali za shughuli za Umoja huo nchini Tanzania.
Mtaalam
wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce
Temu akitoa maelezo kwa mwananchi katika picha za viongozi mbalimbali
waliowahi kuwa Makatibu wakuu wa Shirika la Umoja Mtaifa duniani ambalo
hivi sasa linaongozwa na Ban Ki-Moon.
Pichani
juu na chini ni Ismael Mnikite (kushoto) kutoka kituo cha Habari cha
Umoja wa Mataifa (UNIC) akitoa maelezo ya shughuli mbalimbali
zinazofanywa na mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa nchini kwa
wananchi waliotembelea banda la Umoja wa Mataifa katika maonyesho ya 39
ya kimataifa ya biashara ‘Sabasaba’, ndani ya viwanja vya Mwl. J.K
Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
Mtaalam
wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce
Temu (katikati) akifafanua jambo kwa mdau wa Umoja wa Mataifa, Shaweji
Steven (kushoto) aliyetaka kujua zaidi kuhusiana na ushiriki wa Umoja wa
Mataifa katika tatizo la ajira za vijana nchini. Kulia ni Emmanuel
Johnson kutoka Shirika la Afya (WHO) nchini.