Jul 14, 2015

UCHAWI WATAWALA TASNIA YA FILAMU

 MSANII wa filamu Tanzania Elia Daniel ‘Elly G’

MSANII wa filamu wa kiume Elia Daniel ‘Elly G’ amefunguka kwa kusema kuwa baadhi ya wasanii wana wivu katika tasnia ya filamu kwa kiwango kikubwa hata kufikia kuwaroga wale ambao wanaonyesha juhudi zao katika fani hiyo, Elly G anadai kuwa kuna wakati ambao wawapo Lokeshini hutokewa mauzauza.

“Kuna baadhi ya wasanii hawataki kabisa kuona unafakiwa katika tasnia ya filamu Bongo, utaona msanii akiona tu kila wakati upo Lokesheni unashuti halafu kazi nzuri zinakubalika na jamii tatizo na vichomi utapata tena rafiki yako,”anasema Elly G.

Msanii huyo anayefanya vinzuri katika tasnia ya filamu katika uongozaji na uigizaji anasema anawashauri wasanii wenzake badala ya kuwa na wivu wa chuki wawe na wivu wa kimaendeleo ili tasnia isonge mbele na si kudumaa, ushindani kwake anaona ni muhimu sana katika kufikia ndoto zake.
FC