Meneja
Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando akiongea wakati wa ufunguzi
wa semina elekezi ya Airtel Rising Stars kwa viongozi wa mikoa
iliyofanyika leo (Julai 7, 2015) jijini Dar es Salaam. Katikati ni
Mwenyekiti soka la vijana wa TFF Ayoub Nyenzi na Kushoto ni Mwenyekiti
msaidizi soka la vijana wa TFF Khalid Abdallah.

Mkurugenzi
wa ufundi wa TFF Salim Madadi akiongea wakati wa wa semina elekezi ya
Airtel Rising Stars kwa viongozi wa mikoa iliyofanyika leo (Julai 7,
2015) jijini Dar es Salaam. Katikati Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania
Jackson Mmbando akifatiwa na Mwenyekiti soka la vijana wa TFF Ayoub
Nyenzi.

Viongozi
soka kutoka katika mikoa inayoshiriki michuano ya Airtel wakifatilia
Seminar elekezi ya Michuano ya Airtel Rising Stars iliyofanyika
iliyofanyika leo (Julai 7, 2015) jijini Dar es Salaam. Mikoa
inayoshiriki katika michuano ya mwaka huu ni pamoja na ya Mwanza,
Morogoro, Mbeya, Temeke, Ilala and Morogoro kwa upande wa wasichana huku
mikoa ya Ilala, Kinondoni, Temeke, Mbeya, Mwanza and Arusha ikiwa ni
kwa upande wa wasichana.

Mwenyekiti
soka la vijana wa TFF Ayoub Nyenzi akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa
Semina elekezi ya michuano ya Airtel Rising Stars iliyoshirikisha
wasimamizi na viongozi wa mikoa itakayoshiriki katika michuano ya Airtel
Rsing Stars inayotegemea kutimua vumbi 20 Julai. Kushoto ni Meneja
Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando na kulia ni baadhi ya
viongozi wa TFF.
Shirikisho
la Soka nchini (TFF), limewasisitiza viongozi wa soka ngazi za mikoa
kutambua kuwa lengo kuu la michuano ya Airtel Rising chini ya vijana wa
miaka 17, ni kuibua vijana kwa manufaa ya Taifa kwa baadaye na sio
kulelekeza nguvu zao katika kupata matokeo mazuri uwanjani kama ambavyo
watu wengi hufikiri.
“Tumegundua
kwamba baadhi ya viongozi wa soka mikoani wana fikra tofauti na lengo
la michuano hii, wao huangalia zaidi kupata matokeo mazuri uwanjani
kuliko kutafuta vijana wenye vipaji kama lilivyo lengo la michuano hii.
Na hii ndio sababu kuu ya ongezeko la tatizo la watu kuleta vijana
waliozidi umri uliolengwa katika program hii”, amesema.