Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na
Utalii, Dkt. Adelhem Meru ( kulia) akiwa
na Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Miradi la Ujerumani la Giz nchini Tanzania, Dkt. Sussane Grimm ( kushoto)
wakitia saini hati ya Makubaliano ya kusimamia na kuendeleza Maliasili nchini.
Hafla hiyo fupi ilifanyika Jijini Dares Salaam, Makao Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Mpingo House.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,
Dkt. Adelhem Meru ( kulia) akiwa na Naibu
Mkurugenzi wa Shirika la Miradi la
Ujerumani la Giz nchini Tanzania, Dkt. Sussane Grimm ( kushoto)
wakibadilishana hati ya Makubaliano ya usimamizi na uendelezaji wa Maliasili nchini. Hafla hiyo fupi ilifanyika
Jijini Dares Salaam, Makao Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Mpingo
House.
Serikali ya Ujerumani kupitia Shirika la
Miradi la Ujerumani la Giz la nchini Tanzania imetia saini hati ya makubaliano na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii katika
kuendeleza na kusimamia Maliasili zilizopo nchini.
Hati hiyo ya Makubaliano imesainiwa na
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Adelhem Meru na Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Giz nchini Tanzania, Dkt. Sussane Grimm .
Utiaji saini huo umefanyika Jijini Dares salaam, Makao Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii,
Mpingo House, na kushuhudiwa na
Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori , Bw. Herman Keryaro pamoja na baadhi
ya Maafisa wa Wizara hiy.
Serikali ya Ujerumani kupitia Shirika la
Miradi la Ujerumani la Giz
nchini Tanzania imeongeza kiasi cha Euro million tatu sawa na billion kumi kwa pesa za Kitanzania katika kusaidia
usimamizi wa kiufundi ikiwemo
uanzishwaji wa Mamlaka ya Wanyamapori nchini Tanzania ( TAWA) . Pia Makubaliano hayo yatadumu kwa muda
wa miaka mitatu katika kusimamia na
kuendeleza Maliasili nchini.
Uhusiano
kati ya Serikali ya Ujerumani kupitia Shirika la Miradi la
Ujerumani la Giz nchini Tanzania na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na
Utalii ulianza mwaka 2014.
Pia
Shirika la Miradi la Ujerumani la Giz
nchini Tanzania imekuwa ikishirikiana
na Serikali ya Tanzania kupitia Wizara
ya Maliasili na Utalii katika kipindi cha mpito cha Uanzishwaji wa Mamlaka ya
Wanyamapori ( TAWA) katika kuwandaa
watumishi kufanya kazi katika Mamlaka
hiyo
na JIACHIE