Mwenyekiti
wa Chamacha Albino Tanzania (TAS), Bw. Ernest Kimaya (kushoto) akiwa na
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda
wakati wa maadhimisho ya Siku ya Walemavu wa Ngozi Tanzania kwenye
viwanja vya Garden Mjini Iringa Mei 4, 2010.

Mwenyekiti
wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (Albino) ndugu Ernest
Kimaya akimfariji Mama Maria Chambanenge wakati akipatiwa matibabu
katika hospitali kuu ya Mkoa Rukwa kufuatia kukatwa mkono wake wa
kushoto na watu walioshirikiana na mume wake na ambao walitiwa mbaroni
na polisi mwaka 2013.

Mwenyekiti
wa Chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (Albino) Ernest
Kimaya akisisitiza jambo kwa wanahabari kufuatia kuvamiwa na kukatwa
mkono kwa Mama Maria Chambanenge wa mkoani Rukwa Februari 19, 2013.

Mwenyekiti
wa Chama cha Albino Tanzania, Ernest Kimaya, akitoa nasaha zake wakati
wa maadhimisho ya Siku ya Watu wenye Albinism Duniani katika Uwanja wa
Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Juni 13, 2015. 

Rais
Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma, wakiwa na Bw. Kimaya wakiwasikiliza
watoto wenye albinism wakiimba wakati wa maadhimisho ya Siku ya Watu
wenye Albinism Dunia kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha
Juni 13, 2015.
Mwenyekiti
wa TAS, Ernest Kimaya, akimpokea Rais Kikwete katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Kilimanjaro Juni 12, 2015. Rais Kikwete ndiye aliyekuwa
mgeni rasmi wa maadhimisho ya Siku ya Watu wenye Albinism Duniani jijini
Arusha 2015.
Mwenyekiti
wa Chama cha Albino Tanzania Bw. Ernest Kimaya akisoma nakala za Katiba
Inayopendekezwa yenye maandishi yaliyokuzwa mara baada ya kukabidhiwa
na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro Machi 15, 2015.
na JIACHIE