Jul 1, 2015

Mfuko wa uwekezaji wa pamoja wazinduliwa nchini

 Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Core Securities Limited, Bw. George Fumbuka akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Umande Unit Trust (UTT), mfuko wa uwekezaji wa pamoja utakaowawezesha wakezaji wengi kukusanya mitaji yao kwa pamoja ili kupata mtaji mkubwa zaidi. Ameambatana na Meneja uendeshaji wa kampuni hiyo Bw. Jonathan Swalala (Kulia) na Meneja Mahusiano ya Wawekezaji, Bi. Sandra Felician (kushoto). UUT ni mfuko wa pili wa pamoja kusajiliwa nchini, kufuatia mfuko ulio chini ya serikali unaojulikana kama Dhamana ya uwekezaji Tanzania (UTT). 
Meneja uendeshaji wa kampuni ya Core Securities Limited, Bw. Jonathan Swalala akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Umande Unit Trust (UTT), mfuko wa uwekezaji wa pamoja utakaowawezesha wakezaji wengi kukusanya mitaji yao kwa pamoja ili kupata mtaji mkubwa zaidi. Ameambatana na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Bw. George Fumbuka (wa pili kushoto) na Meneja Mahusiano ya Wawekezaji, Bi. Sandra Felician (kushoto). UUT ni mfuko wa pili wa pamoja kusajiliwa nchini, kufuatia mfuko ulio chini ya serikali unaojulikana kama Dhamana ya uwekezaji Tanzania (UTT).

Kampuni ya Core Capital Securities imezindua mfuko wa uwekezaji wa pamoja uitwao Umande Unit Trust, utakaowawezesha wakezaji wengi kukusanya mitaji yao kwa pamoja ili kupata mtaji mkubwa zaidi.

UUT ni mfuko wa pili wa pamoja kusajiliwa nchini, kufuatia mfuko ulio chini ya serikali unaojulikana kama Dhamana ya uwekezaji Tanzania (UTT).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa UUT Bw. George Fumbuka alisema kuwa wawekezaji wamepatiwa njia nyingine iliyo salama na rahisi zaidi itakayowawezesha kuwekeza fedha zao.

“Faida ya uwekezaji hutokana na ukubwa wake, yaani mtaji mkubwa huzaa faida kubwa zaidi. Lakini pia hutokana na kusambazwa kwake katika mirija kadha wa kadha ya uwekezaji,” alisema.