10:10 Bado kikao cha Kamati Kuu (CC) kinaendelea taarifa
zilizopo ni kwamba kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC)
kimeahirishwa hadi kesho saa nne asubuhi
8:12 Kikao cha Kamati Kuu kinarudi kuendelea na
kitatoa taarifa ya majina matano ambayo kwa sababu ya muda yatajadiliwa
kesho na Kikao cha Halmashauri na Mkutano Mkuu utafanyika kesho mchana,
Kwa mujibu wa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
7:00 Kamati Kuu ya CCM imeeenda mapumziko mafupi kwa ajili ya Kufuturu na watarejea tena majira ya saa mbili usiku.
4:30 KUMEKUCHA Dodoma, Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeanza mkutano wake wa Kamati Kuu saa chache zilizopita.
Taarifa kutoka Dodoma zinasema watu wote
wameondolewa ndani ukumbi mpya wa CCM ikiwa ni pamoja na waandishi wa
habari ambapo hivi sasa wanasubiri taarifa hizo nje ya ukumbi huo.
Endelea kuwa nasi kwa habari zaidi kutoka Dodoma ......
