Jul 11, 2015

Kamati kuu yaendelea na kikao

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiendelea na mkutano wake mjini Dodoma 

10:10 Bado kikao cha Kamati Kuu (CC) kinaendelea taarifa zilizopo ni kwamba kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kimeahirishwa hadi kesho saa nne asubuhi
8:12 Kikao cha Kamati Kuu kinarudi kuendelea na kitatoa taarifa ya majina matano ambayo kwa sababu ya muda yatajadiliwa kesho na Kikao cha Halmashauri na Mkutano Mkuu utafanyika kesho mchana, Kwa mujibu wa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.

7:00 Kamati Kuu ya CCM imeeenda mapumziko mafupi kwa ajili ya Kufuturu na watarejea tena majira ya saa mbili usiku.
4:30 KUMEKUCHA Dodoma, Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeanza mkutano wake wa Kamati Kuu saa chache zilizopita.
Taarifa kutoka Dodoma zinasema watu wote wameondolewa ndani ukumbi mpya wa CCM ikiwa ni pamoja na waandishi wa habari ambapo hivi sasa wanasubiri taarifa hizo nje ya ukumbi huo.
Endelea kuwa nasi kwa habari zaidi kutoka Dodoma ......