Mkurugenzi wa Sheria wa Kampuni
ya Bia Tanzania (TBL), Bw. Stephen Kilindo (kulia), akikabidhi mfano wa
hundi ya Dola 24,000 za Kimarekani kwa Meneja wa Fedha na Utawala wa
Taasisi ya ACE Afrika, Bw. Oswald Mwita, Dar es Salaam jana kwa ajili ya
kuongeza tija kwa wakulima wa mbogamboga na wafugaji wa mbuzi wa maziwa
katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Mwanza. Fedha hizo zimetolewa na
Kampuni SABMiller tanzu ya TBL.
Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia
Tanzania (TBL), Dorice Malulu (kulia), akifafanua jambo kuhusu msaada
uliotolewa na Kampuni hiyo kwa ACE Afrika kwa ajili ya kuongeza tija kwa
wakulima wa mbogamboga wa mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Mwanza.
Wengine ni Meneja wa Fedha na Utawala wa ACE Afrika, Bw. Oswald Mwita
(kushoto) na Mkurugenzi wa Sheria TBL, Stephen Kilindo.
Meneja wa Fedha na Utawala wa
Taasisi ya ACE Afrika, Bw. Oswald Mwita, akizungumza na waandishi wa
habari Dar es Salaam jana baada ya kupokea mfano wa hundi ya Dola 24,000
za Marekani zilizotolewa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kwa ajili
ya kuongeza tija kwa wakulima wa mbogamboga katika mikoa ya Arusha,
Meneja wa Fedha na Utawala wa
Taasisi ya ACE Afrika, Bw. Oswald Mwita, akizungumza na waandishi wa
habari Dar es Salaam jana baada ya kupokea mfano wa hundi ya Dola 24,000
za Marekani zilizotolewa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kwa ajili ya
kuongeza tija kwa wakulima wa mbogamboga katika mikoa ya Arusha,
chanzo GPL