SHUGHULI MBALIMBALI ZA WAZIRI MKUU KWA MIKOA YA ARUSHA NA DODOMA
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mbunge wa
Ukonga Eugen Mwaiposa kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Juni 3,
2015. Wengine pichani kutoka kushoto ni Kaimu kiongozi wa Upinzani
Bungeni, Tundu Lisu, Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa, Katibu Mkuu
Kiongozi Balozi Seif Sefue na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Galawa.

Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dkt. Seif Rashid baada ya kuhudhuria sala na heshima za mwisho kwa
aliyekuwa mbunge wa Ukonga, Egin Mwaiposa kwenye viwanja vya Bunge mjini
Dodoma Juni 3, 2015.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Wakufunzi na watalaam wa mashine za
kuandikisha wapiga kura za BVR wakati alipotembelea Kituo cha mafunzo ya
BVR kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Juni 2, 2015
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi
za Jamii, NSSF, Dr. Ramadhani Dau, jijini Arusha Juni 3, 3015. Juni 2,
Mheshimiwa Pinda alifungua Mkutano wa tano wa wadau wa NSSF.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema
(kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko la Hifadhi za jamii, NSSF, Dkt.
Ramadhani Dau mjini Arusha Juni 3, 2015. Juni 2, Mheshimiwa Pinda
alifungua Mkutano wa Tano wa Wadau wa NSSF. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)