Balozi
wa Marekani nchini Tanzania Mark Childress akizungumza katika uzinduzi
wa mradi wa PROTECT wa dola za kimarekani Milioni 14.5 wa kulinda
mazingira,kukuza uhifadhi na utalii nchini hapa unaolenga kujenga uwezo
wa uhifadhi na kukabiliana na ujangili na usafirishaji haramu wa
wanyamapori nchini kote Tanzania,uzinduzi huu ulifanyika jana katika
eneo la hifadhi ya wanyamapori linalosimamiwa na jumuiya ya uhifadhi ya
wanyamapori {WMA} la Randilen linalopakana na hifadhi ya taifa tarangire
Wilayani Monduli mkoani Arusha.
Balozi
wa Marekani nchini Tanzania Mark Childress wakitiliana saini mkataba wa
mradi wa PROTECT na Waziri wa Mali Asili na Utalii nchini Tanzania
Lazaro Nyalandu
Waziri
wa Mali Asili na Utalii nchini Tanzania Lazaro Nyalandu akizungumza
katka uzinduzi huo, ameishukuru serikali ya Marekani kwa msaada huo huku
akiongeza kuwa kumekuwa na uvamizi mkubwa katika maeneo ya hifadhi za
taifa na kusema kuna mpango makakati wa kuhakikisha njia zote
zinafunguliwa ili kuwezesha wanyamapori wote kuwa huru kuzunguka katika
hifadhi zote nchini.