Jun 15, 2015

MWILI WA MUFTI KUSAFIRISHWA KESHO MKOANI SHINYANGA.

Mufti ,Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba enzi za uhai wake.
 Sehemu ya wanawake waliofika nyumbani kwa Marehemu  Mufti Alhaj Sheikh Shabaan Issa Bin Simba Mikocheni B jijini Dar es Salaam leo.
Sheikh  Mkoa wa Dar es Salaam,Alhaj Sheikh Alhad Mussa Salum akibadilishana na mawazo na Sheikh wa Mkoa wa Kigoma Hassan Kiburwa walipofika nyumbani kwa Marehemu Mufti ,Mikocheni B leo jijini Dar es Salaam .

Kulia ni Sheikh wa Mkowa Dar es Salaam,Alhaj Sheikh Alhad Mussa Salum akiwa na baadhi ya Masheikh waliofika Nyumbani kwa Marehen Mufti,Shabaan Issa Bin Simba Mikocheni B Jijini Dar es Salaam.(PICHA NA EMMANUEL MASSAKA.)

Na Chalila Kibuda.
MWILI wa  Mufti ,Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba unatarajiwa kusafirishwa kesho mkoani Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata),Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam,Alhaj Mussa Salum amesema mwili wa marehemu utaswaliwa kesho katika Msikiti wa Msilimu ,viongozi mbalimbali wa dini na serikali watakuwepo.

Amesema marehemU alikuwa akisumbuliwa na sukari,Shinikizo la Damu (BP)  pamoja na Figo.

Hata hivyo amesema kuwa jana (Jumapili) Mufti alifanyiwa oparesheni ya figo katika Hospitali ya TM Jijini Dar es Salaam na Mauti ya Mufti yamekuta majira ya saa moja leo.

Salum amesema marehem anatarajiwa kuzikwa Alhamis mkoani Shinyanga.
 
habari na jiachie blog