Wananchi
wa Mji wa Kigoma wakiwa wamejipanga kando ya Barabara kuu ya Kutoka
Ujiji, kumpokea Mtangaza nia ya Kuwania Urais kwa tiketi ya CCM, Mh.
Edward Lowassa.
Mtangaza
nia ya Kuwania Urais kwa tiketi ya CCM, Mh. Edward Lowassa akiwapungia
mkoani wana CCM pamoja na wananchi wa Mji wa Kigoma waliofika kumlaki
kwenye Ofisi Kuu za CCM mkoani hapo.
Mh.
Lowassa akisani kitabu cha wageni kwenye Ofisi Kuu za CCM Mkoani Kigoma
leo, Kulia ni Mjumbe wa Mkutano Mkuu (NEC), Daniel Nsanzugwanko.
Waziri
Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM
mkoa wa Kigoma, Dkt. Aman Kaborou, muda mfupi kabla ya kupokea idadi ya
majina ya wanaCCM waliomdhani ili apate ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi
kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika
Oktoba 25, 2015. Mh. Lowassa amedhaminiwa na wanaCCM 11,250 Mkoani
Kigoma, leo Juni 13, 2015.
Wazee kwa vijana wakimshangilia Mh. Edward Lowassa.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinganga, Hamis Mngeja akizungumza machache mbele ya hadhara ya wanaCCM wa Mkoa wa Kigoma.
Katibu
wa CCM Wilaya ya Kigoma Mjini, Noverty Kibaji akizungumza wakati
akimuelezea Mh. Lowassa, idadi ya wanaCCM waliomdhani ili apate ridhaa
ya Chama kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa
kufanyika Oktoba 25, 2015.
Katibu
wa CCM Wilaya ya Kigoma Mjini, Noverty Kibaji (kushoto) akimkabidhi,
Mh. Edward Lowassa, majina ya wanaCCM wa Kigoma Mjini waliomdhani ili
apate ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi kuwania Urais wa Tanzania kwenye
Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.
Mh.
Lowasaa akionyesha majina ya WanaCCM wa Mkoa wa Kigoma waliomdhani ili
aweze kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi kuwania Urais wa Tanzania.
Mjumbe wa Mkutano Mkuu (NEC), Daniel Nsanzugwanko (kulia) amkabidhi Mtangaza nia, Majina ya wanaCCM wengine waliomdhani.
Umati
wa WanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Kigoma, ukiwa umefurika kwenye
Uwanja wa Ofisi Kuu ya CCM Mkoa wa Kigoma, kuja kumuona Mh. Edward
Lowassa (anaeonekana kule mbele) wakati alipofika kuomba udhamini wa
wanachama wa CCM, ili aweze kupata ridhaa ya Chama kuwania Urais wa
Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.
Mh. Lowassa amepata udhaminiwa na wanaCCM 11,250 wa Mkoa wa Kigoma, leo
Juni 13, 2015.
Mh. Edward Lowassa akizungumza na WanaCCM wa Mkoa wa Kigoma.
chanzo na JIACHIE BLOG