
Mratibu
wa Bima ya Elimu kwa Uwapendao kutoka Taasisi ya Kifedha ya Bayport
Financial Services, Ruth Bura, kushoto akimkabidhi hundi Latifa Juma
yenye thamani ya Tsh 3,000,000, baada ya mzazi wake Juma Said, aliyekuwa
Mchapa Vitabu wa Shule ya Uhuru Mchanganyiko, jijini Dar es Salaam.
Kulia ni mume wa Latifa, anayeitwa Bakari Msumi. Picha zote kwa Hisani
ya Bayport Financial Services.
Bayport
Financial Services yamfuta machozi Latifa Said
TAASISI ya
Kifedha ya Bayport Financial Services, leo jioni imemkabidhi hundi ya Sh Milioni
tatu (3,000,000), mjasiriamali Latifa Juma, ikiwa ni sehemu ya mafao yake baada
ya mzazi wake Said Juma, kuwa mteja wa Bayport kwa kupitia huduma yake ya Bima
ya Elimu kwa Uwapendao iliyoanzishwa mapema mwaka jana.
Makabidhiano
hayo yalifanyika Makao Makuu ya Bayport Financial Services, Morocco, jijini Dar
es Salaam, huku akisindikizwa na mumewe Bakari Msumi. Akizungumza
katika makabidhiano hayo, Mratibu wa Bima ya Elimu kwa Uwapendao ya Bayport
Financial Services, Ruth Bura, alisema kwamba marehemu Said Juma alikuwa mteja
wao, huku akijiunga pia katika huduma ya bima, ambayo leo imemnufaisha mtoto
wake.
Mratibu
wa Bima ya Elimu kwa Uwapendao kutoka Taasisi ya Kifedha ya Bayport
Financial Services, Ruth Bura, kushoto, akiwa kwenye makabidhiano ya hundi
Latifa Juma yenye thamani ya Tsh 3,000,000, baada ya mzazi wake Juma
Said, aliyekuwa Mchapa Vitabu wa Shule ya Uhuru Mchanganyiko, jijini Dar
es Salaam. Kulia ni mume wa Latifa, anayeitwa Bakari Msumi. Picha zote
kwa Hisani ya Bayport Financial Services.
