Mashuhuda wa tukio hilo wanasema kuwa mlipuaji wa bomu hilo la kujitolea muhanga alikuwa amelenga wanajeshi wa kimataifa nje ya lango kuu la uwanja huo wa ndege.
Lango hilo hutumika na vikosi vya kijeshi vya kigeni. Kundi la Taliban limethibitisha kuhusika na shambulio hilo katika taarifa yake lililoituma kwa wanahabari.
Shambulizi hilo linafanyika ikiwa ni siku tatu baada ya mwanamgambo mmoja wa Taliban kuwaua watu 14 wakiwemo raia tisa wa kigeni katika hoteli moja mjini humo.
Chanzo: BBC