Mkuu
wa mkoa wa Dar es slaam,Saidi Meck Sadiki(katikati) akiangalia athari
ya maji yaliyotokana na mvua kubwa zilizonyesha hivi karibuni jijini Dar
es slaam akiwa ameambatana na wakazi wa eneo hilo la Kunduchi
Ununio.Manispaa ya Kinondoni kwa kushirikiana na DAWASA inaendelea na
zoezi la kuyaondoa maji hayo pamoja na ujenzi wa mfereji mkubwa kuelekea
baharini utakaokusanya maji kutoka Bunju na Kunduchi na kuyapeleka
bahari ya Hindi.
Kazi ya ujenzi wa mfereji huo mkubwa wenye urefu wa kilometa 2.1 ikiendelea katika eneo la Kunduchi Ununio.
Maji
yaliyotuama yakiwa bado yamezingira nyumba na makazi ya watu eneo la
Boko jijini Dar es salaam ambayo harakati za kuyaoondoa zinaendelea
kufanywa na manispaa ya Kinondoni.
Mkuu
wa mkoa wa Dar es salaam, Said Meck Sadiki ( katikati ) akisikiliza
maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni Musa Nati wakati
akikagua utekelezaji wa zoezi la kuondoa maji katika makazi ya watu eneo
la Basihayo Tegeta.