Filamu ya “Anko Kiepe” Imeingia Leo Sokoni
Filamu kali na ya kusisimua ya Anko Kiepe imeingia
sokono leo tarehe 11 na imesambazwa nchi nzima hivi karibuni akiongelea
filamu hiyo mungozaji na mtunzi wa filamu hiyo Phelimon Lutwaza anasema
kuwa ni kazi ya kipekee na anaonyesha uwezo wake kwa kufanya maajabu
makubwa.
“Anko Kiepe inakuja kufanya mapinduzi makubwa katika tasnia ya filamu
Bongo Movie nimefanya mambo makubwa sana katika sinema hii kiuigizaji
shutingi na wasanii wameitendea haki sinema hii, pia nimeiongoza
mwenyewe,”anasema Lutwaza.
Filamu ya Anko Kiepe imewashirikisha wasanii nyota kama Patcho
Mwambo, Phelimon Lutwaza, Yobnesh Yusuf na wasanii wengine wanaofanya
vinzuri katika tasnia ya filamu na filamu hiyo inasambazwa na kampuni
ya B.M.O nunua nakala halisi kukuza vipaji vya wasanii wa Tanzania.
chanzo: bongo movies.com