Mar 3, 2015

Shamsa: Sijaachana na Mume Wangu

Mrembo na mwigizaji wa filamu Shamsa Ford amewafungukia watu wanaoeneza taarifa kuwa ameachana na mumewe, Dickson Matoke kwamba hakuna kitu kama hicho.
Uvumi wa Shamsa kuachana na mumewe umechangiwa hasa na Shamsa mwenyewe kutokan na “posts” anazoweka mtandaoni kwa siku za hivi karibuni, kwani zimekuwa kiziongelea maswala ya mapenzi na hasa swala la kutendwa katika mapenzi huku akiwasifia wanawake kwa moyo wao wa kupenda na kuweka picha zaidi akiwa na mototo wake pekee na kusema  hiyo ndio furaha yake, tofauti na zamani ambapo alikuwa akiwepa picha akiwa na mume wakepamoja na motto na kuandika maneno ya upendo.
Akizungumza na gazeti moja hivi juzi kati, Shamsa alisema kuwa hajaachana na mumewe huyo na wote wanaosema hivyo watakuwa wanamtaka.“Bado nipo na mume wangu tena kajaa tele, nashangaa hao wanaosema kuwa tumeachana labda wanamtaka,” alisema Shamsa.