Kampuni ya Zanzibar Media Corporation ambayo ni wamiliki wa Zenji Fm Radio na gazeti la Nipe
Habari, kesho Ijumaa tarehe 27 February wanatarajia kutoa tuzo kwa wasanii bora wa Zanzibar.
Akizungumza na
gazeti hili Mratibu wa tuzo hizo Nd Said Khamis amesema jumla ya
washiriki 76 wameshindania katika vipengele 20, na washindi wa vipengele
hivyo wanatarajiwa kupewa tuzo na fedha taslim.
Aidha Said
ameongeza kuwa tuzo hizo ambazo ni za 8 kufanyika mara hii zimeonesha
kuwa kuna mwamko kwa wasanii wa Zanzibar kwa kuweza kutengeneza kazi
nzuri na zenye ushindani katika tasnia ya musiki wa Zanzibar.
Sherehe hizi
ambazo zitafanyika katika ukumbi wa Salama Bwawani,mgeni rasmi
anatarajiwa kuwa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Dk Mwinyi Haji
Makame.
+255 777 468189