Mwaka 2014, Beyonce peke yake aliingiza zaidi ya dola milioni 115 na Jay Z aliingiza zaidi ya dola milioni 60 na hivyo si kitu cha kushangaza kama wanandoa hao wenye nguvu wakitoa dola milioni 85, kununua mjengo wa kifahari uliopo huko, Beverly Hills estate.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, Bey bna Jay wameonekana kwenye nyumba hiyo kwa zaidi ya mara sita na wana nafasi kubwa ya kuinunua. Wakala wa masuala ya nyumba Branden Williams amekadiria kuwa nyumba hiyo inaweza kuuzwa kwa dola milioni 70 na wawili hao wanatarajia kukamilisha malipo kabla ya Christmas.’
Nyumba hiyo ina vyumba vinane, mabafu 13 na ina garage ya kuegesha magari 16.