Nov 13, 2014

ORIJINO KOMEDY KUKAMUA TAMASHA LA TIGO JIJINI MWANZA

Msanii wa Kundi la Orijino Komedy, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’  (katikati) akielezea jinsi kundi lake litakavyofanya makamuzi kwenye tamasha hilo. Kushoto ni Isaya Mwakilasa ‘Wakuvanga’ na Lukas Mhuvile ‘Joti’, kulia ni Meneja wa Bidhaa za Tigo, Edwin Mgoha na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Farid  Kubanda ‘Fid Q’.

Meneja wa Bidhaa za Tigo akisistiza jambo.
Masanja Mkandamizaji  akilonga na wanahabari (hawapo pichani).
Wanahabari wakiwa kazini.
Msanii wa Orijino Komedy, Mujuni Silvery ‘Mpoki’ (kulia) akiahidi kufanya makuu kwenye tamasha hilo. Kulia ni Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Mwana FA akifuatiwa na  Mac Reagan wa Orijino Komedy.
Mac Reagan akijaribu kuonesha mambo anayotarajia kwenda kuyafanya kwenye tamasha hilo.
Masanja Mkandamizaji, Wakuvanga (kushoto) na Joti (aliyesimama) wakionesha mbwembwe zao.
Joti na Young Killer wakiwa kwenye pozi.
KUNDI  la vichekesho la Orijino Komedy kwa kushirikiana na wanamuziki wa kizazi kipya akiwemo, Farid Kubanda ‘Fid Q’ na Young Killer, keshokutwa Jumamosi wanatarajia kutoa burudani ya nguvu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza kwenye tamasha liitwalo Welcome Pack ambalo limeandaliwa na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo.
Akizungumza kwenye mkutano na wanahabari uliofanyika leo katika ofisi za Tigo zilizopo Kijitonyama Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Bidhaa za Tigo, Edwin Mgoha, alisema katika tamasha hilo kiingilio kitakuwa ni laini ya tigo ambapo wateja watakaofika watapata maelekezo ya huduma mbalimbali za mtandao huo.
(PICHA NA RICHARD BUKOS / GPL)