Rais wa nchi ya China, Xi Jinping akiwapa mkono wananchi wa Tanzania.
Inadaiwa kuwa wanunuzi, raia wa Uchina walinunua maelfu ya kilo za
pembe za ndovu nchini Tanzania na kuzitorosha kutoka nchini humo katika
ndege ya kibinafsi ya raia wa Uchina Xi Jinping wakati alipozuru bara
Afrika.Kulingana na shirika la ujasusi la mazingira lililo na makao yake
mjini London.
Ndege ya rais wa China.
Pembe hizo zilinunuliwa wiki moja tu kabla ya ziara ya rais huyo wa
Uchina nchini tanzania mwaka ulioipita ambapo zilifichwa katika mifuko
ya wanadiplomasia ili kutokamatwa.
Shirika hilo pia linadai kwamba wajumbe waliokuwa wakiandamana na Rais Xi walinunua viwango vikubwa vya pembe hizo.
Pembe za ndovu.
Uuzaji wa Pembe za ndovu ulipigwa marufuku mwaka 1989 ili kuwazuia wawindaji haramu kuwaua ndovu.
(CREDIT: BBC SWAHILI)