
Naibu
Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele (wa pili kushoto)
akimwongoza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Mohamed Gharib Bilal (wa pili kulia) kutoka eneo la mkutano katika
Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa AICC mara baada ya ufunguzi wa
Kongamano la Tano la Kimataifa ambalo linajadili masuala mbalimbali kuhusu matumizi ya nishati ya jotoardhi kwa nchi wananchama kwa nchi zilizo katika bonde la ufa na nchi nyingine duniani. Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo na Mkurugenzi wa
Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais Julius Ningu (wa kwanza kulia).
Kongamano la Tano la Kimataifa ambalo linajadili masuala mbalimbali kuhusu matumizi ya nishati ya jotoardhi kwa nchi wananchama kwa nchi zilizo katika bonde la ufa na nchi nyingine duniani. Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo na Mkurugenzi wa
Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais Julius Ningu (wa kwanza kulia).

Sehemu
ya Washiriki wanaohudhuria Kongamano la tano la Kimataifa la Jotoardhi
kwa nchi zilizo katika bonde la Ufa katika ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wakifuatilia hotuba ya ufunguzi kutoka kwa Makamu wa Rais
Dkt. Mohamed Gharib Bilal.

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohamed Gharib Bilal
(katikati) akifuatilia taarifa kuhusu Kongamano la Tano la Kimataifa la
Jotoardhi, wengine kutoka kushoto ni Kamishna wa Miundombinu na Nishati
kutoka Umoja wa Nchi za Afrika Dkt. Elham Ibrahimu, Naibu Katibu Mkuu
Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava, Naibu wa Nishati na
Madini anayeshughulikia Madini Stephen Masele, Mkurugenzi Mtendaji wa
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Mazingira kwa Ukanda wa
Afrika (UNEP), Mounkaila Goumandakoye, Naibu Waziri anayeshughulikia
masuala ya nishati wa Iceland Einar Gunnarsson na Mkuu wa Mkoa wa Arusha
Magesa Mulongo.

Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Mhandisi Ngosi Mwihava,
akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Gharib Mohamed Bilal mara baada ya kufungua Kongamano la Tano la
Kimataifa la Jotoardhi.

Baadhi
ya Washiriki wa Kongamano la Tano la Kimataifa la Jotoardhi katika
picha ya Pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. Mohamed Gharib Bilal baada ya kufungua kongamano hilo.

Naibu
Waziri anayeshughulikia masuala ya Nishati, Einar Gunnarsson akitoa
taarifa kwa ufupi kuhusu namna nchi hiyo ilivyoendelea katika masuala
ya nishati ya Jotoardhi. Imetajwa kuwa nchi ya Iceland ni miongoni mwa
nchi zilizoendelea katika nishati hiyo.

Naibu
Waziri wa Nishati na Madini Stephen Masele akipata maelezo kuhusu
masuala ya jotoardhi katika moja ya mabanda aliyoyatembelea mara baada
ya kufungua Maonesho ya kuhusu masuala ya jotoardhi zikiwemo bidhaa na
teknolojia zinazotumika katika nishati hiyo.

Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya kuendeleza Jotoardhi Tanzania, Mhandisi Boniface
Njombe (wa kwanza kushoto mwanzo) akiongea jambo na baadhi ya wageni
waliotembelea banda la Kampuni hiyo. Kampuni hiyo ya Jotoardhi
ilianzishwa mwaka 2014 .
Nishati ya Jotoardhi inakua Afrika- Bilal
Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Mohamed Gharib Bilal amesema ni wakati muafaka kwa Tanzania kuongeza vyanzo vya nishati ya umeme ikiwemo vitokanavyo na nishati ya jotoardhi kutokana na umuhimu wake kwa maendeleo ya kiuchumi, vilevile kutokana na Tanzania kuwa na hazina kubwa yenye viashiria vya jotoardhi.
Ameongeza kuwa, nishati ya umeme ni miongoni mwa maeneo ya
kipaumbele ya Serikali kuhakikisha taifa linakuwa na nishati ya
kutosha ya umeme, ya uhakika na nafuu kutokana muhimu wa nishati hiyo
kwa maendeleo ya kiuchumi, kiviwanda na katika sekta ya kilimo na
kwamba ni chanzo cha nishati kisichokwisha.
Aidha, Makamu wa Rais amezitaka nchi wananchama zilizo katika bonde la
ufa na nchi nyingine za Afrika kutumia fursa zinazotolewa na
Mashirika ya Kimataifa na Taasisi zilizobobea katika masuala ya
jotoardhi kuviendeleza vyanzo hivyo katika nchi zao kwa maendeleo ya
nchi hizo.
Kongamano hilo limefunguliwa leo tarehe 29 Oktoba, 2014 na
kuwashirikisha washiriki zaidi ya 400 kutoka nchi wananchama kutoka
katika bonde la Ufa na nchi nyingine duniani, zikiwemo taasisi za
Kimataifa zinazohusika na masusla ya jotoardhi na nchi nyingine
zilizopiga hatua katika nishati hiyo ikiwemo Iceland na litaendelea
hadi tarehe 31 Oktoba,2014.