Jul 18, 2014

TAMASHA LA MATUMAINI 2014 WABUNGE SIMBA NA YANGA KUONESHANA KAZI

Talk of the town kwa sasa ni tamasha kubwa na la kipekee, Usiku wa Matumaini linalotarajiwa kutimua vumbi Agosti 8, 2014 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambalo ukiachilia mbali burudani kibao zitakazokuwepo, mechi kati ya wabunge wanaoishabikia Yanga dhidi ya wale wa Simba inatarajiwa kuwa kivutio cha aina yake.

Wabunge wa timu ya Yanga wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Kama ilivyokuwa kwenye tamasha hilo mwaka jana ambapo Rais Kikwete alipuliza kipyenga kuashiria kuanza kwa mtanange huo, waheshimiwa kibao wataoneshana uwezo wao dimbani kwa kusakata kabumbu safi kumsaka mshindi.
Ukiachilia mbali gemu hiyo ya kipekee, kivutio kingine kitakuwa ni mechi ya soka kati ya Bongo Fleva na Bongo Muvi ambao nao watachuana vikali kumsaka mshindi.

NDONDI
Burudani nyingine itakayolipamba tamasha hilo ni ndondi ambapo mabondia Mada Maugo na Thomas Mashali watavurumishiana makonde ulingoni kumtafuta mbabe, kwa upande wa wabunge, Mwigulu Nchemba atadundana na Hamis Kigwangala, Bongo Muvi, Jackob Steven ‘JB’ atazichapa na Issa Musa ‘Cloud 112’ na wengine wengi.
Wabunge wa timu ya Simba wakiwa kwenye picha ya pamoja.
BURUDANI YA MUZIKI
Mkali wa ngoma ya Johnny, Yemi Alade kutoka nchini Nigeria naye atatimba nchini kwa lengo moja tu, kukinukisha kwenye Tamasha la Matumaini. Listi ya wasanii wa Bongo ni ndefu wakiwemo Ali Kiba, Roma, Madee, Juma Nature na kruu nzima ya Wanaume Halisi, Madee na Wema Sepetu ambaye ameahidi kuimba na kucheza nyimbo za bebi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond’.

Tamasha la Usiku wa Matumaini linaletwa kwenu kwa udhamini mkubwa wa Vodacom, Azam TV, E. FM na Times FM, hii siyo ya kukosa!