WEKUNDU
wa Msimbazi, Simba wamekamilisha usajili wa kipa namba moja wa Mtibwa
Sugar, Hussein Sharrif `Iker Casillas` na kumsainisha mkataba wa miaka
miwili.
Kwa
muda mrefu Simba ilionesha nia ya kumsajili mlinda mlango huyo bora wa
ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita, lakini ilimkosa mara kadhaa
na sasa ndoto zimetimia.
Casillas aliyekuwa tegemeo katika klabu ya Mtibwa Sugar ameungana na makipa Ivo Mapunda na Abuu Hashim katika kikosi cha Simba.
Simba
ilimtema kipa wake, Mghana, Yaw Berko baada ya kumalizika kwa msimu wa
2013/2014 wa ligi kuu Tanzania bara, hivyo kubakiwa na makipa wawili tu.
Kusajiliwa
kwa Casillas ambaye aliwahi kuitwa katika kikosi cha Taifa stars chini
ya Kim Poulsen kutaleta upinzani mkubwa baina yake na kipa namba moja wa
Simba, Ivo Mapunda.
Uwezo
mkubwa aliouonesha kwa wakati wote akiidakia Mtibwa Sugar, Casillas
anatarajiwa kuisaidia Simba inayohitaji mafanikio msimu ujao.
Wakati huo huo, Simba imemsainisha kipa kinda, Peter Manyika Junior ili ajiunge na Simba B.