May 13, 2014

ALBINO AUAWA, ACHUKULIWA VIUNGO VYAKE HUKO SIMIYU

  Mwili wa marehemu Nughu Lugata ulivyokutwa

Mguu wa marehemu Nughu Lugata ukiwa umekatwa.

MAREHEMU Nughu Lugata ambaye ni albino ameuawa na viungo vyake kuchukuliwa na watu wasiojulikana jana majira ya saa moja jioni huko Bariadi mkoani Simiyu.

Nughu ameuawa kwa kukatwa mapanga na baadhi ya viungo vyake kama mguu wa kushoto na vidole vitatu kuchukuliwa na watu wasiojulikana.

Marehemu alikuwa mkazi wa Gasuma akijishughulisha na kilimo.