Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao lao kwa kucheza kiduku.
Emanuel Okwi wa Yanga akifunga daluga lake.
Timu zikiingia uwanjani
Mpambano kati ya Yanga SC na Azam FC uliopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam hivi punde, umemalizika kwa matokeo ya bao 1-1. Bao la Yanga limefungwa na Didier Kavumbagu katika dakika ya 14 kipindi cha kwanza wakati la Azam likiwekwa kimiani na Kelvin Friday dakika ya 38 kipindi cha pili.
VIKOSI VILIKUWA HIVI;
KIKOSI CHA YANGA SC
Juma Kaseja, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub "Cannavaro", Kelvin Yondani, Frank Domayo, Saimon Msuva, Hassan Dilunga, Didier Kavumbagu, Hamisi Kiza, Emmanuel Okwi.
KIKOSI CHA AZAM FC
Aishi, Nyoni, Michael, Morad, Balou, Himid, Sure Boy, Friday, Bocco, Kipre Tchetche na Mcha.
na http://www.globalpublishers.info