Nov 12, 2013

JK AZINDUA SHULE YA MWEKEZAJI MZALENDO SEKTA YA MADINI.


 Shule hii imegharimu kiasi cha shilingi milioni 460 hadi kukamilika kwake ina vyumba saba vya madarasa ya kisasa, jengo kubwa la utawala, maktaba moja, nyumba saba za walimu, matundu manne ya vyoo vya walimu, matundu 24 ya vyoo kwaajili ya wanafunzi na thamani za ofisi na madawati.






Rais Jakaya Kikwete amezindua shule ya msingi ya Ng'anzo iliyojengwa na mwekezaji mzalendo wa sekta ya madini (dhahabu) Emmanuel Gungu ambaye ni mmiliki na Mkurugenzi wa Kampuni ya NGASALI LTD.