Sep 21, 2013
MAUAJI YA KINYAMA MWANZA KATA YA BUHONGWA
Usiku wa kuamkia leo jijini Mwanza, kata ya Buhongwa kumetokea mauaji ya
kinyama. Mauaji hayo yamefanywa leo saa kumi usiku. Watu wa tatu wa
familia moja akiwemo Mtoto wa miezi saba (7) waliuwawa kikatili, kwa
kunyongwa, ndani ya nyumba yao na watu wasiojulikana. Kwa habari za
awali ni kwamba, watekelezaji wa mauji hayo walifanikiwa kuingia ndani
ya nyumba hiyo pasi na kuvunja mlango. Licha ya nyumba ya marehemu hao
kuzungukwa na nyumba zingine. Hata hivyo hakuna aliyefanikiwa kutoka ama
kusikia wakati unyama huo ukiendelea. Kila aliyeulizwa alisema hajui
chochote juu ya tukio hilo. Mama na mtoto wa miezi 7 walinyongwa, baba
akachinjwa! Miili ya marehemu hao bado ipo ndani ya nyumba ikisubiri
uchunguzi zaidi. Askari nao wamefika eneo la tukio na uchunguzi
unaendelea.